Namna ya kubadilisha jezi na nembo Dream League #Team Logo and kits.


Baada ya kuangali namna ya kupata sarafu (coins) na wacheza bora (classic players) bure, leo hii tunakuja na maujanja ya namna ya kuweka au kubadilisha jezi na nembo ya timu yako na kuweka upendayo (kama Manchester United, Real madrid, Barcelona na nyinginezo nyingi).
Je unajisikiaje kuwa unalazimika kutumia jezi na nembo ya timu usiyopenda?
Bila shaka hamna apendae! Dream League 2017 ni moja kati ya magemu pendwa sana na wengi wetu, wakubwa na wadogo! Wa kike  na kiume! Lakini,
Swali linalowaumiza wengi wetu ni kwanamna gani ntaweka nembo na jezi ya timu ninayoipenda?

Bila kupoteza mda tuanze moja kwa moja...

Chagua na copy link ya jezi au nembo (logo) unayo taka kupitia link ya hapo chini..

Pata link za nembo na jezi za timu unayotaka. #Team logos and kits

1. Fungua gemu lako na elekea katika kipengele cha my club.


 2. Elekea kwenye kipengele cha customize Team.

3. Chagua Edit kit (kwa upande wa jezi).


 4/. Chagua delete kama unataka kubadilisha iliyopo.


 5. Chagua Download (Pakua).

 6. Paste link unayotaka katika nafasi itakayo pewa.

7. Kisha ponyeza download. 
Rudia kuanzia step ya 5 mpaka ya 7 ukishamaliza save marekebisha.

Kufikia hapo utakuwa umeshabadilisha jezi za timu yako.

Katika upande wa nembo ya timu (logo) nayo pia ni rahisi.
1. Chagua Edit logo



2. Chagua download
Ukisha chagua download kinachofuata, paste link ya logo unayotaka Kisha download na save mabadiliko ya gemu uliyoyafanya.

Ukisha maliza marekebisho yote save tena kiujumla gemu lako na Kisha endelea kufurahia na mchezo.
Je unaionaje hii? Je wewe ni mmoja kati ya waliokuwa wanahitaji kubadilisha nembo na jezi ya timu yako?
Ni magemu gani mengine ungependa kupata maujanja kama haya? Tuandikie hapo chini.
Kumbuka kusambaza Upendo.

Comments :

  1. in my phone is error 512x512 are comming logo size is not work. can you tell me how to solve this problem. i am awating your reply admin
    thanks dream league soccer kits

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hello,
      can you please share a screenshot here or send an email to mtatiromagoiga@gmail.com

      Delete

Post a Comment

write to us your views on this

Interested to get more of our Update !